CHAMA cha Soka mkoa wa Kagera (KRFA), kimempinga Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodegar Tenga na kamati yake ya utendaji kwa kupinga mchakato wa marekebisho ya Katiba ya shirikisho hilo.
Mwenyekiti wa KRFA, Jamali Malinzi amesema kuwa katika kikao cha kamati yake ya utendaji kilichoketi Desemba Mosi mjini Bukoba wamekubaliana kutoshiriki mchakato wa marekebisho hayo ya katiba yanayoendeshwa kwa njia ya waraka na kudai kuwa ni batili.
"Mchakato wa TFF wa kubadili katiba ya TFF kama ulivyoanishwa katika warakata wa TFF kwa vyama wanachama wake ni batili kwa kuwa haukidhi matakwa ya katiba ya TFF kifungu cha 22 (1). Kifungu hicho cha 22 kinasema kuwa mkutano mkuu wa TFF ndio pekee wenye mamlaka ya kubadili katiba ya TFF, aidha kifungu kidogo cha 30 1-6 kinaeleza taratibu nzima ya mchakato wa kubadili katiba ikiwa ni pamoja na kutoa notisi ya siku 45, kuitisha mkutano mkuu na kupigak ura na wajumbe theluthi mbili kuridhia.
"Hakuna mahali popote kwenye katiba ya TFF panapotamka kuwa katiba ya TFF itabadilishwa kwa wanachama kuzungushiwa waraka kupiga kura na kuandika jina na saini na kisha kuituma kura makao makuu ya TFF sisi kama KRFA hatutashiriki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...