Luton Tanzanian Community (LTC) Uingereza Kwa kushirikiana na Tripple EM Inawaletea Sherehe za Uhuru wa Tanzania na Kenya (Double Celebrations in one) Jumamosi Tarehe 15/12/2012, Roman Way Tomlinson Avenue LU4 0QL - Luton.

Kutakuwa na burudani za kumwaga vichekesho na majonjo ya asilia yetu wana East African Nyama Choma, Tusker na Vyakula asilia vya nyumbani km. Ugali, Kienyeji, Mihogo ya Kuchoma chachandu na Samaki n.k Kiingilio ni Paundi tano tu kabla ya saa sita usiku na baada ya hapo ni Paundi kumi.

Magoma yote ya mwambao na bongo flava na Mayenu kama kawa chini ya ma DJs CYMOH, DJs PAPS, DJs JOE HAMEL na Mtaalam DJs Double T wataangusha magoma kuanzia saa mbili usiku mpaka Majogoo Pia kutakuwa na suprises kubwa ya kutisha siku hiyo usikose.


Watanzania na Wakenya wote UK bila kusahau wana Afrika mashariki wote na marafiki Mnakaribishwa:

      Abraham Sangiwa
…………………………………………..
Katibu - Luton Tanzanian Community.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. '''''''Na tukae kwa undugu amani na undugu!''''''''

    Hicho ni Kipande kidogo ktk Wimbo wa Taifa wa KENYA

    Ni kitu kizuri sana kama kipande cha wimbo hapo juu kinavyosema wana wa Afrika ya Mashariki mkawa pamoja kwa sherehe za Uhuru Tanzania na Kenya!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...