Meneja Mauzo wa Duka la Vodacom Mlimani City, Salim Salmin (Kushoto) akimkabidhi mshindi wa promosheni ya Shinda na Nokia inayoendelea katika msimu huu wa sikukuu, Selemani Methusela, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam zawadi ya Nokia Asha 306. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Duka la Vodacom lililopo Mlimani City Dar es Salaam leo.
Mkazi wa Kibamba, Dar es Salaam, Alfred Mwandika ,akipokea zawadi yake ya T-Shirt toka kwa Meneja Mauzo wa Duka la Vodacom Mlimani City, Salim Salmin (Kushoto) aliyojishindika katika promotion ya Shinda na Nokiamsimu huu wa sikukuu.
Mkazi wa Buza nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, Eusedia Donald, (katikati) akipokea zawadi ya simu aina ya Nokia 302 kwenye duka la Vodacom lililopo eneo la Mlimani City Dar es Salaam leo, kutoka kwa Meneja Mauzo wa duka hilo Salim Salmin (Kulia) kufuatia promosheni ya shinda na Nokia inayoendelea. (Kushoto) ni mwakilishi wa Nokia Magreth Tendwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...