Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel
inayotoa gharama nafuu zaidi Tanzania, leo imegawa sare za shule
pamoja viatu katika shule ya msingi Kiromo iliyopo Bagamoyo mkoa wa Pwani, ikiwa ni
sehumu ya shughuli zao za kusaidia jamii.
Shule ya kiromo ni moja kati ya shule zilizofaidika na mpango wa shule
yetu na kuingia kwenye ukarabati wa majengo na madarasa na kubadili
mazingira ya shule na kutoa vifaa vya kufundishia pamoja na computer.
sasa Airtel imetoa Sare na viatu vya shule kwa wanafunzi wote shuleni
hapo.
Katika kauli iliyotoleawa na kampuni ya Airtel Tanzania kupitia Meneja
shughuli za kijamii bi. Hawa Bayumi alisema” Airtel imedhamiria
kuendelea kuisadia shule mbalimbali kwa kutoa vifaa mbalimbali ikiwepo
vya kufundishia ili kuhakikisha elimu bora inatolewa kwa wanafunzi na
jamii kwa ujumla. Na leo tunaendelea kuboresha shule yetu ya Kiromo
kwa kutoa msaada wa uniform na viatu kwa wanafunzi. msaada wa sare za
shule tunazoto ni pamoja na Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na
viatu 728 vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi
Kiromo.
" Airtel Tunayo malengo ya dhati kabisa katika kusaidia kuinua kiwango
cha elimu hapa nchini na kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka
na upatikanaji wa vitabu kwa wanafunzi wa shule za sekondari. leo
tunathibitisha dhamira yetu ya kusaidia mashule kwa kutoa sare za
shule na viatu Kiromo shule ya msingi”, alisema Bayumi.
Airtel itaendelea kusaidia mashule kwa kutoa vitabu na vifaa mbali
mbali vya kufundishia ikiwa ni sehemu ya shughuli zetu za kusaidia
jamii, nia yetu ni kuwafikia shule nyingi zaidi katika mikoa yote ya
Tanzania aliongeza.
Kampuni ya simu ya Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia
sekta ya elimu hapa nchini. Tangu tulipoanza mradi wa “ shule yetu”
mpango wa kusaidia vitabu na vifaa vya shule , shule mbalimbali
nchini zimeshafaidika na mradi huu mpaka sasa
Meneja wa uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kushoto) akimkabidhi sare za shule Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiromo Nasibu Pangahela mwishoni mwa wiki hii, akishuhudiwa na meneja wa huduma kwa jamii (katikati) bi Hawa Bayumi.
Meneja wa uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kushoto) akimkabidhi mmoja wa wanafunzi wa shule ya msingi Kiromo sare za shule zilizotolewa na Kampuni ya simu ya Airtel mwishoni mwa wiki hii,
akishuhudia makabidhiano hayo (wa pili kushoto) meneja wa huduma kwa jamii bi Hawa Bayumi akifuatiwa na Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kiromo Nasib Pangahela, Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo
Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.
Afisa uhusiano na matukio wa Airtel Tanzania Dangio Kaniki akimvalisha sare za shule na viatu mwananfunzi wa shule ya msingi Kiromo zilizotolewa na Kampuni ya simu ya Airtel mwishoni mwa wiki hii. Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 , skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo
Afisa uhusiano na matukio wa Airtel Tanzania Dangio Kaniki (Kulia) akimpongeza Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Kiromo (kulia) baada ya makabidhiano yaliyofanyika mwishoni mwa wiki hii wakishuhudiwa na
meneja wa huduma kwa jamii wa Airtel Hawa Bayumi (wa pili kulia) akifuatiwa na mmoja wa wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo bi Zuwena Salumu, Airtel metoa msaada wa sare za shule zikiwemo Kaptura 600 ,
skirt 600 , mashati 1193 na viatu 728 vyote vyenye dhamani ya shilingi milioni 50 kwa shule ya msingi Kiromo.
Tafadhali rekebisha usemi maana sielewi Dangio ni nani na Mwalimu Mkuu ni nani maana wanaonekana wote wapo upande wa kulia kutokana na maelezo.
ReplyDelete