CHAMA cha mpira miguu Dar es Salaam(DRFA), kimejipanga kukutana na wanachama wake wa mkoa huu, ili kujua kiundani jinsi wanavyoendesha shughuli zao, kwa maana ya ufanisi, mikakati yao, chang’amoto walizonazo na nini kifanyike ili matarajio yanayokusidiwa yafike kwa wakati mwafaka.

Uongozi mpya tuliongia madarakani Desemba mwaka jana, tuna kila sababu ya kufanya yale ambayo kila mmoja wetu alidhamiria katika sera zake za kujinadi, hivyo hatuwezi kukurupuka, bila kwanza kukutana moja kwa moja na wanaoguswa na changamoto mbalimbali za uendelezaji soka mkoani Dar es Salaam na kuona ni jinsi gani DRFA inaweza kusaidia au kuchangia maendeleo na utatuzi wa changamoto mbalimbali.

Katika mkakati huo, Februari 8, tutakutana na chama cha waamuzi mkoani(FRAT Dsm), kujadili kwa kina idara yao na changamoto zake kwani wao ni watu muhimu sana katika kufikisha dhamira za kweli ya uendelazaji wa mchezo huu mkoani kwetu. Februari 9, DRFA itakutana na viongozi wa chama cha soka wilayani Ilala(IDFA), pia kwa makusudio hayohayo.

Chama cha soka wilayani Kinondoni (KIFA), siku yao itakuwa Februari 10 na ratiba hiyo itaendelea kwa vyama vingine shiriki kadri tutakavyo panga. Vyama hivyo ni pamoja na Chama cha Soka la Wanawake (DWFA) sanjari na Chama cha Mpira miguu wilayani Temeke (TEFA), ambao hawajajibu wito wetu, lakini iwapo tu watafanya hivyo, kutakuwa na kikao nao.

Februari 12 mwaka huu, kutakuwa na kikao cha pili cha kamati ya utendaji, pamoja na mambo mengine kupokea taarifa za mikutano yote ya wadau tuliokutana nao na kuangalia nini kifanyike kwa maslahi ya soka la Dar es Salaam.

Tunatanguliza shukrani
Msanifu Kondo.
Katibu Mkuu DRFA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...