Wazir wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa akionyeshwa Mfumo wa Maji Taka na Meneja Mazingira Bw Dominick Mariki wakati  Waziri alipofanya Ziara ya Kutembelea Kiwanda cha  Bia cha Serengeti Breweries cha  Jijini Dar es Salaam ambacho Wananchi wanakilalamikia kinawamwagia Maji Machafu katika Mtaa wa Chamwenyewe Chang'ombe.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Terezya Huvisa akimsikiliza Operesheni Meneja wa Kiwanda cha Bia cha Serengeti Shekhor Mokosare, Waziri  alifanya  Ziara ya kukagua na kuangalia  Uchafuzi wa Mazingira  Unaofanywa na Kiwanda cha Bia cha Serengeti cha Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk Terezya Huvisa akimsikiliza Bi Mwaka Washokela kuhusu Malalamiko ya Umwagaji wa  Maji Machafu ya  Kiwanda cha Bia cha Serengeti katika Mtaa wa Chamwenyewe, Chang'ombe Jijini Dar es Salaam.Picha na Ali Meja
-
Wito umetolewa na Waziri wa Mazingira ofisi ya makamu wa Rais Bibi Terezya Huvisa kwa wenye viwanda na Hoteli za kitalii kote nchini kuzingatia usafi wa mazingira sababu mazingira ni uhai. Alitoa rai hiyo wakati wa ziara yake iliyofanyika jijini Dar es Salaam kwa kutembelea baadhi ya viwanda na Hoteli za kitalii.

Viwanda alivyotembelea ni pamoja na Serengeti Breweries

Kiwanda kingine alichotembelea Waziri ni kiwanda cha kuchapisha maandishi kwenye fulana  na vipeperushi ambacho kinaitwa CI Group kilikutwa na makosa mabalimbali ikiwamo uchafu wa mazingira ya kiwanda kwa ujumla, mazingira wanayofanyia kazi wafanyakazi wa kiwanda ni machafu sana hivyo kupelekea afya zao  kuwa hatarini.  Hata hivyo wamiliki wa kiwanda hicho walikimbia baada ya kumuona Waziri na ujumbe wake wakiwasili. Bibi Huvisa ametoa agizo kwa watu wa NEMC kwenda kukifunga kiwanda hicho mara moja.

Waziri Huvisa pia alitembelea hotel mbalimbali katika  maeneo ya Oysterbay ambapo wameagizwa kuwasilisha cheti cha mazingira, na  kama hawana hatua za kisheria zitachukuliwa ikiwamo Hotel kufungwa. 

Mwisho Waziri amewataka wenye Hotel kutilia mkazo swala zima la kutibu maji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Seacriff, Golden Tulip, Police Mess na Coco beach nadhani zote zimekiuka sheria za mita 60 toka ufukweni. Coco ni ya walala hoi kwahiyo itafungwa tu,Police Mess ni serikali kwahiyo...., Seacriff na Golden tulip ni za wanene na uwekezaji mkubwa umewekwa na wahusika walikuwa wapi wakati zinajengwa. Si haki kufungwa wakati watu wahusika walisha bugi men. Sasa Slipway na double tree, mbalamwezi nk. itakuwaje.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...