Kampuni ya bia ya Serengeti inaendelea kufanya kampeni maalumu kwa msimu wa valentine kwa wapenzi wa kinywaji cha Baileys kwa kutoa zawadi mbalimbali kwa wateja wao zawadi hizo zinatolewa katika supermarket za Mlimani City, Uchumi na Shoppers Plaza kwa wale watakaonunua baileys wanapata t-shirt, maua, chupa ya Baileys na kubwa zaidi ni kupata bahati ya kula chakula cha jioni katika mgahawa wa kisasa wa Akemi uliopo jijini Dar es Salaam.
 Katika picha ya pamoja Thomas Michelis akiwa na mke wake baada ya kukabidhiwa ua kutoka Baileys ishara ya upendo
 Thomas Michelis akisoma kipeperushi na kupata maelekezo kutoka kwa balozi wa kinywaji cha baileys katika supermarket ya Shoppers Plaza, kuhusu kinywaji hicho na zawadi zinazotolewa  katika msimu huu wa Valentine
Meneja masoko wa vinywaji vikali kutoka kampuni ya bia ya Serengeti  Emillian Rwejuna akiwaelezea wanahabari jinsi kampeni hiyo inayofanyika katika supermarket mbalimbali huku akionyesha baadhi ya zawadi ambazo wapenzi wa Baileys wanapata.
Mteja wa Baileys akijaribu bahati yake katika msimu wa valentine ndani ya supermarket ya Shoppers Plaza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...