Na Mahmoud Ahmad,Arusha
TANZANIA imepata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika kupitia vivutio vyake bora vya utalii vya  Mlima Kilimanjaro,Hifadhi ya Ngorongoro na Hifadhi ya Serengeti ambayo ndio iliongoza kwa kupata kura nyingi kuliko nchi nyingine yeyote.
Akitangaza matokeo hayo jana mjini hapa  rais wa taasisi iliyoandaa tuzo hiyo Dk. Phillip Imler wa Marekani mbele ya waziri mkuu Mizengo Pinda alisema sababu iliyopelekea Tanzania kupata ushindi huo  ni kutokana na  kuwa na vivutio vya kipekee.
Akielezea hifadhi ya taifa ya Serengeti alisema kuwa ndio hifadhi ya kipekee iliyopata kura nyingi na kutokana na tabia za misafara ya wanyama wanaohama kwa msimu maarufu kama annul animal migration.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliyekuwa mgeni rasmi katika ghafla hiyo, alisema kuwa nchi za Afrika zina vivutio vingi vya utalii na fursa kubwa ya kukuza pato kupitia utalii huo.
Alisema kutokana na sifa ambayo Tanzania imezipata kupitia vivutio vyake vitatu itaendelea kuvitunza kuhakikisha kuwa  vinavutia zaidi watalii na kuongeza pato la taifa.
“Afrika ina vivutio vingi  vyenye kuvutia hivyo kila nchi ni lazima ijivunie rasilimali hizo kwa kuvitunza na kuviendeleza,”alisema
“Kwa Tanzania ni bahati ya pekee kwa kuweza kupata tuzo tatu za maajabu saba ya Afrika  ambazo ni za Mlima Kilimanjaro, Bonde la Ngorongoro pamoja na hifadhi ya Taifa ya Serengeti hivyo ni wajibu wa kuvitunza na kuviendeleza,”alisema Pinda.
Aliongezea  kuwa iwapo watanzania wataendeleza tabia ya utunzaji wa vivutio vilivyopo nchini, nchi itaendelea kupata sifa duniani kote.
Naye Mkurugenzi wa Hifadhi za Taifa,(TANAPA),Dkt.  Alan Kijazi alisema mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu barani Afrika na hivyo una kila sababu ya kushinda na watanzania waendelee kuutunza.
Dkt Kijazi alisema kuwa hifadhi hiyo imeshinda kwa kuwa kuwa na wanyama wa kila aina kama Big Seven, Simba, tembo, Viboko, Nyati, Vifaru, Sokwe na Mamba.
Mbali na Tanzania Dk.Imler alivitaja vivutio vingine vilivyoshinda kuwa ni Red sea Reefs, Okavango Inland  delta iliyopo nchini Botwasana, Sahara Desert na River Nile.
Aidha Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki alisema ushindi huo ni historia kubwa duniani na kwamba ni jambo la watanzania wote kujivunia.


Pia aliwashukuru wananchi walioshiriki katika mchakato mzima wa kupiga kura na kuviwezesha kuingia katika ushindi kwa mara tatu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa


  1. S A L U T E ! ! !

    ReplyDelete
  2. KWA MANTIKI HIYO, TANZANIA INATAKIWA KUSHIKA NAFASI YA TATU KWA MAENDELEO YA KIUCHUMI BARANI AFRIKA.

    ReplyDelete
  3. Namshukuru muumba kwa kunipa nguvu na uwezo wa kutembelea sehemu zote tatu na nyingine pia.

    ReplyDelete
  4. Hii ni fursa ya kuanza kujitangaza kabla hali haijapoa maana kuna msemo unasema MCHUZI WA MBWA UNANYWEWA UNGALI MOTO, tutabaki tunapongezana tunasahau majukumu ya kufanya promotion

    ReplyDelete
  5. Hongereni sana watanzania wenzangu!

    ReplyDelete
  6. WATANZANIA TUNATAKIWA KUWA WATALII NCHINI MWETU LAKINI GARAMA ZIKO JUU SANA.BODI YA UTALII FANYIA HILO KAZI. MASHULE YAMEJITAHIDI KUPELEKA WANAFUNZI KUTALII LAKINI BADO WAZAZI INAKUWA NGUMU SANA KUKABILI GARAMA HIYO

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...