Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji DKT. Mary Nagu (katikati) akifurahia jambo na viongozi wa makampuni ya china (kushoto) ni Mkuu wa chama cha ushirikiano cha China Bw. Charles Li wakiwa wanaonyesha bango lenye maandishi ya lugha ya China kuonyesha ushirikiano kati ya China na Tanzania (kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi wa WCUGA International Group Bw. Tiger Liang.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Nchini (TIC) Bw. Raymond Mbilinyi (kushoto) akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji, DKT. Mary Nagu wakielekea katika ukumbi wa kivukoni katika Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam juzi jioni kuonana na ujumbe wa wawekezaji wa china kwa ajili ya kujadili namna ya kuangalia fursa mbalimbali za uwekezaji hapa nchini. Ujumbe huo wa makampuni kumi na tano toka nchini China uliongozwa na Mkuu wa chama cha ushirikiano cha China Bw. Charles Li.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...