Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Balozi Thomas Winkler kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na Denmark katika masuala ya  sheria na mikataba mbalimbali  ya kimataifa ikiwemo masuala ya kupambana na Uharamia. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 20 Machi, 2013.
Balozi Winkler akichangia hoja wakati wa mazungumzo hayo huku Balozi Kasyanju akimsikiliza.
Balozi Kasyanju akimsikiliza Balozi Winkler wakati wa mazungumzo yao. Wengine katika picha ni Bw. Elisha Suku (kulia), Afisa Mambo ya Nje katika Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje, Bi. Mille Sofie Brandrup (kushoto), Afisa kutoka Idara ya Sheria za Kimataifa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark na Bw. Lars Bo Kirketerp Lund, Afisa kutoka Ubalozi wa Denmark hapa nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...