Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaocheza soka la Kulipwa nchini Congo DRC katika Timu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu (kushoto) na Mbwana Samatta wakizungumza na mmoja wa mashabiki wa Soka nchini Tanzania aliyewalaki walipo wasili uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana tayari kwa kujiunga na kambi ya Timu ya Taifa ikiwa ni maandalizi ya kuikabili Morocco.
Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaocheza soka la Kulipwa nchini Congo DRC katika Timu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu (kushoto) na Mbwana Samatta wakiwa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili tayari kwa kujiunga na kambi ya Timu ya Taifa ikiwa ni maandalizi ya kuikabili Morocco Jumapili hii katika mechi ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Jamani hebu tuangalie ni vipi tutawa enzi na kuwafurahisha hawa Vijana wetu Mastaa wa Michezo wakiwa wanakuja nyumbani?

    Kwa nini wasipewe nafasi ya kusafirishiwa kwenye ndege na Ma Benzi yao wanayoendesha huko wanakocheza wakija nchini kulitumikia Taifa?

    Sasa, kila usafirishaji wa magari ktk ndege gharama za juu zitozwe na pia tushike Kodi hata kwa hawa wabebaji wa Bendera ya Taifa ?

    Hivyo ndivyo tunavyoweza kuwekeza ktk kuwaamsha ari na mwamko wao wa Uzalendo!!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Pumbalesi hizo pesa za kusafirisha hayo magari. si wapewe watoto yatima hata wao wale vizuri wavae vizuri walale vizuri

      Delete
  2. mdau wa kwanza usirudie tena kuongea upuuzi kama huo ni hayo tu

    ReplyDelete
  3. Mdau wa 2 anony wa Tue Mar 19, 09:22:00 pm 2013

    Wewe ndio umetoa Pumbalesi, Fedha ya kulisha yatima na watoto wa mazingira magumu unatakiwa UCHANGE WEWE pamoja na ZILE LA MAFISADI zikamatwe ndio zitolee huduma hizo!

    Wewe ufanye wizi Serikalini na Fisadi ahujumu mali ya nchi na Serikali, wewe Mwizi wa mali ya umma na Fisadi mtumie fedha zenu kujengea Mabaa na Pubs halafu Star wa Michezo anayeitumikia nchi vyema asipewe heshima yake?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...