Baada ya serikali kutoa siku 30 kwa mjenzi wa ghorofa karibu na lile lililoporomoka na kuua watu zaidi ya 20 siku ya Ijumaa kuu mwaka huu, mtazamo umekuwa tofauti kwa vikwangua anga ambavyo vinazidi kume akila kona kama uyoga. Serikali pia imeziagiza halmashuri za Dar es salaam za Ilala, Kinondoni na Temeke kutathmini ubora wa ujenzi wa kila ghorofa na litaloonekana limejengwa chini ya kiwango libomolewa...
Maeneo ya Gerezani. Uwanja wa Kidongo Chekundu juu shuto kuleeeeee...
Maeneo ya Gerezani
Maeneo ya mtaa wa Lumumba Kariakoo. Shoto ni 'Central Park' yetu - Bustani ya Mnazi Mmoja garden
Maeneo ya mtaa wa Ohio kupitia Serena Inn
Dar yapendeza, ila vikwangua anga vingine ninatishia roho zetu
ReplyDeleteDar kwatu, ila vikwangua anga vingine vinatamani roho zetu
ReplyDeleteWatu wangekua wanapaa, ingekuwa poa maana hizo foleni zinatisha na mvua zikinyesha hata barabara hazipitiki. Maendeleo ya ujenzi yaendane sawa na maendeleo ya miundombinu.
ReplyDeleteBarabara hazipo. zinaonekana kama vinjia au njia za wanyama. Hayo maghorofa mnayosifia ndiyo yanayoanguka kwa sababu yapo chini ya viwango.
ReplyDeletekaka Michu leo chopa umeitoa wapi/ Weka angalizo kabisaa hizo picha zina rights wasije watu wakaanza kujibebea tu. Mimi nakutafuta faragha, mambo ya michuziimagebank.com
ReplyDeleteHao wadau wa juu hapo nataka kuwaomba waangalie picha cha New York miaka 50 iliyopita. Halafu watueleze Bongo yetu na hiyo New York bora wapi?
ReplyDeleteAnkal,
ReplyDeleteNext time utuwekee video ya taswira ya Dar-es-Salaam ukiwa ndani ya ndege halafu baadaye unatundika youtube.
Maana hizi still-images za vikwangua anga ingekuwa video clips hakika Dar-es-Salaam kwa juu ni kama New-York City.
Mdau
Kimanzichana
Hivyo ni vikwangua ROHO mbichi za Wananchi.
ReplyDelete