Habari yako ndugu Ankal.
Mimi ni mwanamke, naandika kwenye blog yako natafuta mchumba, kijana ambaye yupo makini na anayetaka kuanzisha familia hivi karibuni. Awe na umri kuanzia miaka 35 mpaka 39. Naomba sana ambao hawako makini kwenye hili swala wasiniandikie.
Rafiki ninayemtafuta awe hajawahi kuoa, awe hana watoto, awe na elimu kuanzia chuo, awe tayari kupima ukimwi, awe mtu wa kumcha mungu (mkristo), mpole, anayejali na mwenye mapenzi ya dhati.
Napatikana kwenye email address:
Dada mchumba nipo hatuna haja ya kuingia gharama ngoma tunapima kwa macho; vifaa vya mchina noma tupu
ReplyDeleteWewe lazima utakuwa kimeo yaani umekosa wanaume mpaka unaamua kutafuta kwenye mtandao, hao wanao kuona kila siku wameshindwa kukutokea kwa ndoa sasa huku kwa ankal ndo itakuwaje??!
ReplyDeleteHizo sifa zote, bado awe single tu?. Lower your expectations Sister.
ReplyDeletekabla hatujaingia kwenye usumbufu wa kuandikiana barua hebu weka picha yako tuangalie usafiri wako na jinsi ulivyo kama pia unalingana na jinsi tulivyo maana siku hizi magari sio injini magari ni shape injini hata likikufia mbele ya safari lakini kwa nje mtu hajui kama bovu
ReplyDeleteAnkal muunganishie na yule jamaa wa Ujerumani aliyekuwa anatafuta mke.
ReplyDeleteunavyoonekana utakua mnoko mnokoooo!halafu unajiskia.
ReplyDeleteKwa sifa anazotaka inabidi akjifanyie promo kanisani sio humu.
ReplyDeleteDada umejitahidi kujitosa hapa! Wapo wengi wanaotafuta wachumba na sababu za vigezo vingi na vikubwa kama hivi ndiyo inasababisha kukosa wa kuishi naye.
ReplyDeleteDomina usijali hizi ndoa tumekaa huko title tu kujiita mama au baba fulani we kula raha kama mambo yako safi jipatie katotoo hata ka kuadopt. Ule raha. Unajitafutia maradhi ya moyo. Asilimia 50 ya ndoa unazoziaona ni majina tu!
wewe dada ni mzima kweli?una shida ya mwenza halafu unaweka masharti kama ya UN?? ndo maana umechina kwa kujidai selective sana.kumbuka mchagua nazi..
ReplyDeleteDa nimecheka sanaaa kwa kusoma maoni na wala si alichoandika huyu dada.anyway goodluck sister in ur mission to find soul mate.
ReplyDeleteKumbe twaweza kufungisha ndoa humu humu, yule jamaa wa miaka 50, alieoa mara mbili, akatapeliwa watoto na mfilipino, sijui mvenezuela anamfaa huyu dada yetu
ReplyDelete