Na Mgendi Boniphace,Mara.

IKIWA Tanzania leo inaungana na ulimwengu mzima kuazimisha siku ya kupinga matumizi ya dawa za kulevya,jamii hususani vijana wametakiwa kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya mbayo yamekuwa yakiathiri nguvu kazi ya Taifa na kuwafanya vijana wengi kuishi katika hali hatalishi.

Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Jamii Information Network linaloshughulika na utoaji elimu katika utambuzi wa mambo mbalimbali yenye kujenga jamii Augustine Mgendi alipokuwa akizungumza na Blog hii namna vijana wengi walivyoathirika kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya.

Amesema vijana wengi ambao ndio tegemeo katika ujenzi wa Taifa wamejitumbukiza katika matumizi ya dawa za kulevya na hivyo kushindwa kushiriki ipasavyo katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo huku wengi wao dawa hizo zikiwatuma kushiriki katika vitendo vya uhalifu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...