Ujumbe wa Chama
cha Ukombozi wa Palestina (PLO) ukiongozwa na Mhe. Tayseer Khalid, Mjumbe wa
Kamati Tendaji na Naibu Mwenyekiti wa PLO ulipotembelea Chuo Kikuu cha Taifa
cha Zanzibar (SUZA) tarehe 13 Juni, 2013. Ujumbe huo ulikuwepo Zanzibar kwa mwaliko
wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambapo Dk. Asha-Rose Migiro, Katibu wa Kamati
Tendaji ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa alifuatana na ujumbe huo. Ujumbe
kutoka PLO pia ulikuwa na Mhe. Bi. Jehad Abu Znead, Mjumbe wa Kamati Kuu ya PLO
(Fateh), Mhe. Dk. Nasri Abujais, Balozi wa Palestina nchini Tanzania na Mhe.
Saleh Rafat, Mjumbe wa Kamati Tendaji ya PLO. Kutoka Zanzibar, ujumbe
ulifuatana na Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Kusini Unguja, Mhe Ramadhan Abdalla
Ali. Baadae ujumbe ulitoa mhadhara kwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar.
Ujumbe wa Chama cha Ukombozi wa Palestina (PLO) ukiongozwa na Mhe. Tayseer Khalid, Mjumbe wa Kamati Tendaji na Naibu Mwenyekiti wa PLO ukitambulishwa kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) tarehe 13 Juni, 2013.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar wakisikiliza wageni
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...