Msemamaji wa Umoja wa wamiliki wa Malori Tanzania, Bwana Elias Lukumay akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya kampuni yake kuhusiana na ongezeko la bima. Kulia kwake ni Makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula.
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa Malori Tanzania, Bi Angellina Ngalula akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na malalamiko ya umoja wao ya kupanda kwa bei za bima kwa asilimia 400. Kushoto kwake ni msemaji wa TATOA, Bwana Elias Lukumay.
========= ======== ======= =========
UMOJA WA
WAMILIKI WA MALORI TANZANIA WALALAMIKIA KUPANDISHWA KWA BEI ZA BIMA
Umoja cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) umelalamikia
ongezeko la bei za bima, ukisema hazijazingatia uhalisia wa soko, pamoja na
kukosa uhalali kwa kuwa hazijashirikisha wadau wa sekta ya usafiri pamoja na
jamii kwa ujumla.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, msemaji wa TATOA
Bwana Elias Lukumay, alisema wanasikitishwa na mamlaka ya uthibiti wa bima
Tanzania (TIRA) kuongeza malipo ya bima kwa asilimia 400 bila kutoa sababu za
msingi lakini pia bila kushirikisha wadau.
‘Majaribio yetu ya kuzungumza na TIRA yameshindika baada ya TIRA
kutojibu barua wala mawasiliano rasmi ya kukutana nao, tofauti na makubalino yetu
ya kikao cha mwezi wa pili, kati yetu na wao ambapo tulikubaliana kuwa na kikao
kabla ya mazungumzo baina ya wadau na umma juu ya swala hili’ alisema Lukumay.
Akielezea zaidi kuhusu malalamiko hayo, Lukumay alisema vigezo
maalumu vya kupandisha bei hizo haviko bayana lakini pia ushindani wa biashara
haukuzingatiwa. ‘TATOA inaamini kuna njia nyingi za kufata ili kupandisha bei,
lakini kubwa zaidi ni kuacha soko lijiendeshe lenyewe, kwani tuko kwenye soko
huria’ alisema Lukumay.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa TATOA, Bi Angellina Ngalula,
alisema ongezeko hili la bei ni kubwa mno kwa mara moja na litapunguza
ushindani wa makampuni ya usafirishaji ya ndani, lakini pia litaongeza bei za
usafirishaji kwa kiwango kikubwa sana na hivyo kuumiza uchumi wa nchi na
mwananchi wa kawaida ataathirika kwa bei za bidhaa kupanda.
‘Sababu za TIRA kupandisha bei sio za msingi, sababu kama
udanganyifu na kuongezeka kwa kesi za bima pamoja na ajali za barabarani, sio
sababu tosha za kupandisha bima kwani kufanya hivyo kutaongeza malalamiko
zaidi, na pia kuwavunja moyo wateja waaminifu’ alisema Bi Ngalula.
Bi Angellina pia alitoa wito kwa wahusika, yaani TIRA, kuacha tamaa
na kutokuendeshwa na genge la makampuni ya bima na kurudi kwenye meza ya
majadiliano ili kuweza kupata muafaka kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi
kwa maendeleo ya taifa.
‘Bila TIRA kurudi kwenye meza ya majadiliano TATOA itabidi ichukue
hatua mbadala kama kwenda mahakamani na kugomea bei hizi mpya, jambo ambalo
litasababisha usumbufu kwenye uchumi wetu’ alisitiza Bi Ngalula.
Bwana Lukumay, asante sana kwa kurudi nyumbani na kusaidia kuinua uchumi wa Taifa kwa njia ya kuanzisha miradi. Umekuwa mfano bora sana kwetu, ingawa sasa unapigwa vita. Panapo majaaliwa siku moja nasi tutarudi. Ila kitendo cha kupandishiwa bima kwa asilimia 400 kwa mpigo! hayo ni mazingaombwe! haijatokea mahali popote hapa duniani. Hii ni hujuma ya wazi wazi isiyo soni, na uroho wa kuchuma pale mtu asipotokwa jasho, pia ni uonevu. Kwani hayo marori yanaanguka kila siku?
ReplyDeleteTunisheni misuli.
Ravi anakusalimia sana.
Wadau CA.
Kwa waliopo nje ya soko la bima kweli watakubaliana na TATOA na kuona wameonewa.
ReplyDeleteIla ukweli wa mambo madai yasiokua ya ukweli (Fake Claims), madai ya kupangwa/kukusudiwa (Moral Hazards) yamekua ni mengi mno katika nchi yetu, walio wengi wamekua wakichukulia bima kama ni njia mojawapo ya kujitajirisha kwa haraka.
Makampuni makubwa ya nje yanayosaidia soko letu kama Munich Re, walijitoa kuhudumia riski zetu kutokana na claim za uongo nyingi.
Sasa kwa mwendo huo si tutauwa soko letu wandugu, tutapeleka wapi riski zetu?
Kama tatoa wataona gharama zimeongezeka, watengeneze mfuko ambao watachangishana, ikitokea mmoja akapata tatizo na asaidiwe kama misingi ya bima ilivoanza kwa wasafirishaji wa majini enzi hizo za kina Llyod.
Ni hayo tu, asanteni wandugu.
Kufuatana na maelezo ya anony wa pili hapo juu mimi basi naomba ku pawepo na uchunguzi kuona tatizo liko wapi. serikali ipo ili ibalance mambo.
ReplyDelete