Mhandisi Adrian Kashula wa VETA Kipawa jijini Dar es Salaam, akitoa maelezo kuhusu teknolojia ya kisasa ya umeme wa viwandani ambayo inatumia eneo dogo na kutoa taarifa pale panapotokea hitilafu, akitoa maelezo kwa wageni waliotembelea banda hilo.
Mwanafunzi wa Mwaka wa Tatu wa VETA Chang’ombe Dar es Salaam, fani ya uchoraji ramani na usanifu majengo, Fatma Mohamedi akitoa maelezo kuhusu mafunzo ya taaluma hiyo yanayotolewa na chuo hicho katika ngazi mbalimbali.
Baadhi ya mashine na mitambo inayozalishwa na vyuo mbalimbali vya VETA nchini, ambayo ikitumika vema inaweza kulikomboa taifa kiuchumi kwa kuepuka utegemezi wa mashine na mitambo kutoka nje.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...