Waziri wa zamani wa Viwanda na Biashara nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), amefutiwa kesi iliyokuwa ikimkabiri yenye  mashtaka manane, likiwemo la matumizi mabaya ya madaraka.

DPP anapoona hana mashahidi thabiti wa kuja kujenga kesi yake anatumia kifungu hicho kufuta kesi kwani kuendelea kuwa na kesi za jinai mahakamani ambazo anaona kabisa hana mashahidi thabiti wa kuwaleta mahakamani ni matumizi mabaya ya sheria na kuisababishia Serikali gharama pamoja na mrundikano wa kesi mahakamani kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini Wakili wa Serikali, Awamu Mbangwa aliwasilisha hati hiyo, chini ya Kifungu cha 91 (1) cha Mashauri ya Jinai (CPA), kwa niaba ya DPP akiomba kesi hiyo ifutwe kwa sababu hana nia ya kuendelea kuwashtaki washtakiwa hao.
Baada ya kuwasilisha hati hiyo.
Hakimu Mugeta alikubaliana na ombi hilo na kuifuta. Mmoja wa mawakili wanaowatetea washtakiwa hao, Alex Mgongolwa alisema hawana pingamizi la kufutwa kwa shauri hilo ingawa walitaka waelezwe sababu za hatua hiyo.
Mgongolwa alisema walitaka kujua sababu hizo kwani walikuwa na wasiwasi kuwa wateja wao wangeachiwa huru na kukamatwa tena baada ya muda mfupi na kupandishwa kizimbani. Kutokana na shaka hiyo, waliiomba Mahakama kuwapa kinga.
Akiifuta kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 3/2013 na kuwaachia huru washtakiwa hao ambao ni Simba na wenzake, Salum Mwaking’inda na Meneja wa Shirika hilo, Victor Milanzi, Hakimu Mugeta alisema maombi ya upande wa mashtaka yamekubaliwa.
Akizungumzia uamuzi huo wa DPP wa kuwafutia kesi wateja wake, nje ya viwanja vya mahakama hiyo, Wakili Mgongolwa alipongeza uamuzi huo akisema ni matumizi ya sheria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 21, 2013

    Tanzania wanafungwa wezi wa kuku na simu za mikononi Mafisadi wanaofilisi Makampuni na Taasisi za Umma hawana makosa wao wanfutiwa Kesi na Kufungwa vifungo vifupi!


    Iba wewe kuku uone?


    Bongo tAMBARALe ,Tanzania jAMBAland ndio kama tuijuavyo!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...