Jirani aliyechonga dili kahama mtaa kwa hofu ya washabiki!

Udaku special, umevuja kutoka katika kambi ya FFU ughaibuni kuwa, Mkuu wa Ngoma Africa band aka FFU,kamanda Ras Makunja atarudishiwa mmoja ya ndege wawili aina ya Bundi aliyokuwa anawamiliki ,uamuzi huo ulitolewa na idara ya uangalizi ya Oldenburg,huko ujerumani.

Mwishoni mwa mwezi wa nne mwaka huu,watu wasio julikana walifanikiwa kuvunja banda walilokuwa wakiishi bundi wawili nyumbani (Anunnaki empire) kwa Ras Makunja na kuondoka na bundi hao wawili,baadaye ndege hao walipatikana katika idara ya uangalizi wa wanyama,na mmoja wao alirudishwa Amerika ya kusini.

lakini mwanzoni wa mwezi julai idara ya wanyama imeamua kumurudisha ndege aina ya Bundi mwenye jina la Udi Udi kwa mmiliki wake ambaye ni mwanamuziki kamanda mkuu Ras Makunja.

Lakini inasemekana kuwa familia ya Kamanda imemtilingia ngumu baba mwenye nyumba kwa kumwambia Bundi hao wasiwekwe ndani ya nyumba bali nje ! .Pia jirani ya Ras Makunja aliyebebeshwa lawama za kuwa ndiye aliyechonga dila na kusababisha Bundi wakamanda wachukuliwe ,Jirani kahama mtaa kwa kuofia baadhi ya washabiki uwenda wakamletea tafrani, Tunamtafuta Kamanda Ras Makunja lakini simu kazima

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 16, 2013

    hiii! Kikamanda ketu ras makunja wamekurudishia bundi wako! sasa naona tour zitakuwa za nguvu sasa

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 16, 2013

    jirani lazima ahame mtaa kwa tabia za washabiki wa ffu

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 16, 2013

    kamanda sijakusikia siku nyingi sana,
    ulikuwa umejichimbia kambini au?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda nakujulisha kuwa waziri mkuu kishakupeni ruhusa ya kupereka virungu popote panapihitajika muziki

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda wale bundi heti uliachiwa na Ayesha G?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 16, 2013

    mkuu kamanda ras makunja nikuulize kitu hivi,hii amri umliopewa na waziri mkuu,mtaichukuliaje ?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 16, 2013

    baba mkuu wa kikosi kazi,mfalume wa viumbe anunnaki,sasa watu wanafuga kasuku wewe unafuga bundi! au ndio unakataa wageni nyumbani

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda tafuta gwanda zako bwana, siyo mambo ya drug and drop.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda waliokuchukulia bundi wako kwanini hukupiga? si mkipewa ruhusa kupiga? au mliogopa nguvu za umma?

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 16, 2013

    Hahahahaha!

    Ama kweli Kamanda Ras Makunja Mkonongo haachi asili yake popote aendapo, ni kuwa unawakilisha Afrika kikweli kweli huko,

    Hadi BUNDI wa Tambiko unaye unafuga?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda Ras Makunja unatakiwa zaidi uende KIDIJITALI!

    Ni kuwa kuanzia sasa unatakiwa uwavalishe ELECTRONIC CHIP hao Bundi wako ili wakiibiwa ujue jinsi ya kuwa track na kuwapata!

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 16, 2013

    Kamanda Makujnas,

    Sio bure!, huyo Jirani yako kama sio M-Benin, atakuwa M-Ghana, M-Guinea,Mu-Ivory Coast, M-Mali,M-Burkina Be wa Burkina Fasso ama M-Senegal wa West Afrika na inawezekana atakuwa na Imani za Kishirikina kwa kuweweseka baada ya kuona NDEGE BUNDI YUPO MJENGONI MWAKO ndani!

    Mnacheza na West Africa?

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 16, 2013

    Mwanawane Majuu kwa Kweli Demokrasia,Ubinaadamu na Haki ipo haswa.

    Yaani mtu unapoteza Bundi Serikali na Manispaa na Serikali za Mitaa wanahakikisha Haki inatendeka na unarudihsiwa ndege wako?

    Bongo acha Bundi kupotea ndio hupati kabisa akipotea ukimpata atakuwa ni Marekemu zamaniiii, ile poteza Paka au Kuku oune kama utampata tena!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 16, 2013

    Ras Makunja utadhani kama yule Mfalme wa Mwisho wa Austria mwaka 1914.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 17, 2013

    Hehehehe!

    Ras Makunjas ameona ya kuwa Mynama Bundi ametengwa sana na jamii kwa kuwa ni nadra sana ukute Bundi amefungwa !, labda iwe ni Kituo cha Utafiti wa Sayansi za Viumbe.

    Hivyo baada ya Mwana wa Makunjas kuliona hilo ilibidi ampe hifadhi ya Kimaisha huyo Bundi akiwa kama Binaadamu anathamini utu wa Viumbe wote, kama alivyofanya Raisi wa Bolivia kupmatia Hifadhi Edward Snowden anatetafutwa na Marekani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...