Pichani juu askari wakikagua mwili wa  Erasto Msuya, mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha aliyejulikana ambaye pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo, baada ya kupigwa risasi na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi na kufa papo hapo.

 Kwa mujibu wa baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walidai kuwa mfanya biashara huyo alifariki dunia mara baada ya majibishano ya risasi baina ya majambazi hayo na mfanya biashara huyo ambapo alizidiwa  nguvu na kupigwa risasi na kufariki dunia

Habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara. 

Habari zaidi tuvute subra kidoogo,
tutazidi kufahamishana kadiri ya taarifa zitakapokuwa zikiingia.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Kuna haja ya jeshi la polisi kuongeza nguvu katika mkoa wa Arusha kutokana na matukio ya uhalifu yanayotokea mkoani humo mara kwa mara

    ReplyDelete
  2. I did loose my uncle Edward Shaba (Mtoto wa marehemu speaker wa bunge Austin shaba ) alipigwa risasi mambo haya ya madini

    ReplyDelete
  3. ano wa 2.
    sorry you did loose your anko to me Edward Shaba was one of my best friends.GOD rest him in peace.
    mikidadi-denmark

    ReplyDelete
  4. Hali si shwari kabisa hapa nchini. Huu wimbo wa ' Amani na Utulivu' has been overtaken by events. Nchi hii sasa ni ya kibedui. Jeshi la Polisi ni usanii mtupu, halafu wanadai wana taarifa za ' kiintelijensia' , when it comes to opposition.
    Hakuna majibu kabisa katika matukio mengi ya ki halifu. Weledi uko wapi?
    It's no longer kisiwa cha amani, wimbo huu uhitimishwe sasa.

    ReplyDelete
  5. Kule Zanzibar husema wanafanya utafiti wa Kisayansi na Tekelakujia.

    Polisi Migwanda kazi yao siasa tu na kulinda Chama.

    Silaha zimezagaa mitaani.

    Muhadhiri kapigwa chuo Kikuu kapigwa risasi. It is just tit for tat.

    Yangelijiri Zanzibar matukio haya. Wangelituita Alqaida Zanzibar nzima.

    Get serious now. Polisi wacheni siasa. Si kazi yenu.

    ReplyDelete
  6. Ni kawaida yetu wananchi kulaumu serikali lakini jee sisi kwa nafasi zetu tunashiriki vipi kulinda amani? Watu wanajua majambazi wanabaki kunyamaza na kuficha siri za wanaomiliki silaha kinyume na sheria. TUSHIRIKIANE JAAMANI HII KAZI YA KUFICHUA MAJAMBAZI SI YA POLISI PEKEYAKE

    ReplyDelete
  7. Arusha has become chaotic jmn....pamekuwa km uwanja wa vita...leo mabomu kesho risasi....achilia mbali watu wa matabaka ya chini ambao wanauwa vinazimwa kimya kimya....enuf iz enuf....its about time that jeshi la polisi wnanchi na serikali kwa ujumla to something to change tht....bila ivo tunapokwenda c pazur
    May Mr. Msuya rest in eternal peace!!

    ReplyDelete
  8. Pole sana kwa wafiwa.
    Hawa watu watafutwe na wawe fundisho kwa wote wanaochukua uhai wa wenzao. Watu wanahenyeka, wao wanawaza jinsi ya kukunyang'anya, wao kujishughulisha hapana. Wanapenda mteremko.
    Kwa Kuwa siku hizi namba za simu zimesajiliwa ni vizuri kutrace namba ya marehemu kwa service providers, wanaweza wakapata namba ya simu ya hayo majangili Kwani walimpigia wakutane sehemu hiyo wakati huo.

    Hakuna haja ya kujisifia kuwa sisi ni watu wa amani kama mwendo ndo huu wa risasi, tindikali, mapanga, sumu, na unyanyasaji usioelezeka unaendelea kuwepo.

    ReplyDelete
  9. Naogopa jamani erasto umeondoka mapema sana
    Mungu akulaze mahali pema peponi

    ReplyDelete
  10. Wengi hawapeleki taarifa Polisi kwani at the end of day zoezi litakubadilikia nawe ukabambikwa uhalifu kwa lengo la kupata rushwa. Nasema hivi, Polisi kumeoza. Garbage in garbage out! Sub standards tupu na udhalimu katika jeshi hili. Wajipange kwani wananchi hawana Imani kabisa na jeshi hili. Ukweli ndio huo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...