Teknoljia ya mstari wa goli  ajili ya Ligi Kuu ya Uingereza imezinduliwa leo na kusifiwa kama moja ya maendeleo muhimu toka sharia za soka ziwekwe na kuanza kutumika miaka 150 iliyopita.

Teknolojia hiyo ijulikanayo kama ‘The Hawk-eye’ (jicho la mwewe) inatumia kamera 14 ambazo zitatuma ujumbe ndani ya sekunde moja katika saa ya mwamuzi pamoja na kifaa cha sikioni cha mawasiliano mara tu mpira utapovuka mstari wa goli.


Watumiaji wa kwanza wa kifaa hicho watakuwa timu za Manchester United na Wigan Jumapili ijayo katika mchezo wao wa ngao ya hisani kuashiria kuanza rasmi kwa ligi hiyo katika uwanja wa Wembley.

Cheki Video hii ya jinsi kifaa hicho kitavyofanya kazi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...