Sheikh Ponda Issa Ponda Akiondoka mahakamani mara baada ya kusomewa mashtaka matatu na kesi yake imehairishwa Hadi  tarehe 28.08.2013
Ulinzi Ukiwa umeimarishwa mahakamani leo 
Sheikh Issa Ponda Akiwa mahakamani mkoani Morogoro asubuhi ya leo Sheikh Ponda Amesomewa Mashtaka Matatu katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro Likiwemo la uchochezi alilolitoa Kwenye  Mkutano wa Hadhara Tarehe 10 mwezi huu ambapo inadaiwa alisema kwamba ”Ndugu waislamu Msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za Misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa Serikali ”katika viwanja vya shule ya kiwanja cha ndege Mkoani Morogoro. Baada ya kusomewa Mashitaka hayo Mahakama imesema Upelelezi Umekamilika na  Dhamana Imefungwa  na Amerudishwa Rumande Mpaka tarehe 28 mwezi huu ambapo kesi hiyo itaanza kusikilizwa katika Mahakama ya Mkoa wa Morogoro..

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Kwa nini Mafaili ya Mtuhumiwa hayakuletwa DSM,mashtaka yakasomewa DSM badala ya kumrusha kwa Chopper(Helikopta) kutoka DSM hadi MRGR na kumrudisha tena DSM kwa Chopper.Wakati mwingine serikali inapoteza pesa bila Sababu za Msingi au sheria hairuhusu?

    David V

    ReplyDelete
  2. naungana nawe!
    huu ni ufujaji wa pesa ya mlipakodi fukara.
    jambo jingine nalaoomba nisaidiwe; kuna yeyete anayeweza kutujuza historia ya huyu bwana!

    ReplyDelete
  3. Aaaa,hata kama historia yake iko namna gani,bado kosa lake si la kuchukuliwa kihivyo,haya yote ni ili kuifurahisha uingereza, cuz the telegraph gazeti la uingereza wanang'ang'ania kuwa ndiye aliye sababisha kumwagiwa tindikali wale waingereza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...