Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera , akifungua jengo la Kompyuta la Chuo cha Uuguzi Berega.
 Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ( watatu kutoka kulia ) walioketi , akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Elias Tarimo ( wapili kutoka kulia)  pamoja na baadhi ya  viongozi wa Kanisa la Anglikana Jimbo la Morogoro , viongozi wa Chuo cha Uuguzi cha Berega , wanafunzi wahitimu wa Diploma na Cheti , mara baada ya kuwatunuku vyeti vyao  Septemba 6, mwaka huu   kwenye  mahafali ya kwanza ya Chuo hicho
 Baadhi ya wahitimu wa uuguzi na ukunga wa ngazi ya Diploma pamoja na Cheti kutoka  Chuo cha Uuguzi cha Berega , kinachomilikiwa na Kanisa la Anglikana Jimbo la Morogoro  wakila kiapo chao  cha kuwauuguzi baada ya kuhitimu masomo yao Septamba 6  mwaka huu.
 Baadhi ya waalimu wa Uuguzi na ukunga wa Chuo cha Uuguzi cha Berega , wilayani Kilosa wakiwa na nyuso za furaha.
CHUO CHA UUGUZI BEREGA KANISA LA ANGLIKANA CHATOA WAHITIMU WA KWANZA .
Picha na Habari na John Nditi).
CHUO cha Uuguzi cha Berega kilichopo Wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro na kumilikiwa na Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Morogoro, kimetoa wahitimu wake wa  kwanza tangu kuanzishwa kwake mwaka 2010 katika masomo ya Stashahada ( Diploma ) na Cheti
Katika mahafali hayo ya kwanza yaliyofanyika Septemba 6,mwaka huu ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera , jumla ya wahitimu 22 walitnukiwa vyeti vyao kati yao 13  ngazi ya stashahada ( Diploma ) ya miaka mitatu na wengine tisa ngazi ya cheti , ambapo  mwaka huu jumla ya wanaunzi 53 wamejisajili kati ya hao 25 ni wasichana na 28 wavulana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jamani basi , kwa kuwa mmeelimika washawishi wenzenu waache kutusi akina mama wanaoenda hospitali kujifungua.

    Hasa wauguzi wa kike.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...