Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Robert Boaz akionesha bunduki iliyokamatwa mbele ya waandishi wa habari(hawako pichani)inayodaiwa kutumika katika mauaji ya bilionea wa madini Erasto Msuya.
Bunduki inayodaiwa kutumika katika mauaji hayo.
Pikipiki mbili zinazodaiwa kutumika katika mauaji ya bilionea wa madini Erasto Msuya.
Picha na Habari nan Dixon Busagaga
wa Globu ya Jamii, Moshi.
JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro limefanikiwa kunasa bunduki aina ya SMG yenye namba za usajili KJ10520 inayoaminika kutumika katika mauaji ya mfanyabiashara bilonea wa madini ya Tanzanaiti , Erasto Msuya (43) aliyeuawa kwa kupigwa risasi 13 kifuani Augosti 7 mwaka huu Mijohoroni wilayani Hai.
Mbali na bunduki hiyo jeshi hilo pia limefanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wengine wanne wanaodaiwa kuwa ni watuhumiwa muhimu katika mipango ya mauaji ya mfanyabiashara huyo anaye aminika kuwa na vitega uchumi vya kutosha katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake,kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro,Robert Boaz,aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni ,Sadick Mohamed Jabir(32) mkazi wa jijini Dar es salaam na Lang’ata
wilaya ya Hai na Karim Issa Kihundwa(33) mkazi wa Lawate wilayani Siha ambao wanatajwa kuwa ni muhimu katika mauaji hayo.
Alisema watuhumiwa hao wawili walikamatwa eneo la Kaliua wilaya ya Sikonge mkoani Tabora wakiwa kwa mganga wa kieneyeji wakifanyiwa zindiko ili wasitiwe mbaroni na baada ya kuhojiwa na polisi walieleza jinsi walivyoshiriki mauaji hayo na mahali walipoficha silaha na pikipiki zilizotumika katika tukio hilo.
Boaz aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Jalila Zuberi Said(28) mkazi wa Babati mkoani Manyara pia anaishi wilaya ya kondoa mkoani Dodoma na Joseph Damas Mwakipesile maarufu kwa jina la ‘Chusa’(35) ambaye pia ni mfanayabiashara wa madini ya Tanzanite anayeishi Jijini Arusha ambaye anashikiliwa na jeshi hilo kwa zaidi ya wiki mbili sasa.
Alisema jeshi hilo pia limefanikiwa kukamata pikipiki nyingine inayodaiwa kutumika katika tukio hilo yenye namba za usajili T751 CKB aina ya KINGLION rangi nyeusi ambayo wakati wa tukio ilikuwa ikitumia namba za bandia.
Kamanda Boaz alisema Bunduki iliyokamatwa ilikutwa ikiwa imefichwa kwneye tindiga katika eneo la Boroi kwenye mpaka wa wilaya za Hai na Siha huku akiendelea kutoa wito kwa wananchi wapenda amani mkoani Kilimanjaro,kuendelea kutoa ushirkiano kwa jeshi hilo katika kukomesha uharifu.
Ni kwa nini RPC ameharibu kesi hii nzuri?Kwa nini asingetumia latent gloves kushika bunduki ili kuhifadhi vielelezo muhimu(yaani alama za vidole-finger prints).Ni watu wangapi sasa watakuwa washika bunduki hiyo pamoja na pikipiki,lo,nasikitika sana!Uharifu hauwezi kupungua au kuisha katika mazingira haya.Ikumbukwe washukiwa watawekewa mawakili kwa gharama za serikali,haoni kwamba watashinda kesi hii kwa kuwa vielelezo muhimu vimeondolewa?Washukiwa wanaweza kupatikana na hati mahakama kuu,lakini wakashinda kesi kupitia rufaa.Ni mpaka lini polisi watabadilika na kuwa makini katika handling exhibits?Kukamata washukiwa na vielelezo ni kazi yao ya msingi,hivyo hawana haja ya kuonyesha,na kama watafanya hivyo,tahadhali tangu ukamataji mpaka kuonyeshwa vielelezo hivyo lazima ichukuliwe kwa umakni mkubwa sana.Naomba wabadilike ili waharifu waadhibiwe kama wanavyostahili.Mwenye mawasiliano na RPC wamjulishe kuwa ameharibu kesi.
ReplyDeleteAisee mimi mwenyewe nimeshangaa sana!Shocking how he is tampering with evidence.
ReplyDelete
ReplyDeleteme ningependa kujua motives za hawa majambazi sasa walimuua kisa hela peke yake au kuna kingine??
alafu mnaposema billionaire wa arusha hivi alikua listed forbes kama billionaire ama wapi?? kuna quaities za kuna billionaire jamani sio kutaja tuu