Msemaji wa Polisi SSP ADVERA SENSO

Tanzania imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika katika utekelezaji wa maazimio ya kikao cha 21 cha wakuu wa polisi Afrika  kilichofanyika Gaborone Botswana mwaka 2011, katika kuzuia na kutanzua makosa yanayovuka mipaka (Transitional Cross Border crimes).
 
Hayo yameelezwa katika kikao cha 22 cha  wakuu wa polisi kutoka nchi za Afrika (Interpol African Reginal Conference) kilichofanyika nchini Algeria kuanzia tarehe 10-12 Septemba, 2013.
 
Miongoni mwa makosa yaliyofanikiwa kudhibitiwa kwa kiwango kikubwa na Jeshi la Polisi kupitia interpol Tanzania na kuiletea sifa nchi ya Tanzania, ambayo yamekuwa yakivuka mipaka ni pamoja na  ugaidi, uharamia, usafirishaji haramu wa binadamu, uzagaaji wa silaha ndogondogo, usafirishaji wa madawa ya kulevya na uingizaji wa dawa bandia.
 
Mbali na azimio hilo, maazimio mengine yaliyokuwa yameafikiwa kutekelezwa yalikuwa ni kuhakikisha kila nchi mwanachama wa interpol anajiunga katika mtambo wa mawasiliano wa interpol, kushiriki oparesheni za pamoja zinazoandaliwa na nchi wanachama na kushiriki katika mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa wa polisi kwa lengo la kupambana na uhalifu, ambayo pia Jeshi la Polisi Tanzania limefanikiwa kuyatekeleza.
 
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Nfikiri madawa ya kulevya hayakuhusishwa katika huo mchakato, vinginevyo tungekuwa wa kwanza kutoka mwisho.

    ReplyDelete
  2. Naona Kamzuzu poa.

    ReplyDelete
  3. Tatizo letu huwa hodari kufanya usanii,ktk madawa ya kulevya,hapo hapana. Watz sasa tunadhalilishwa duniani ktk security checks,hawaangalii mzee/kijana,unatomaswatomaswa mwili wote kama Tonge la ugali,pindi uoneshapo tz passport,hii ni hali mbaya sana. Maofisa wanatakiwa kutoka nje ya nchi,wajionee wenyewe,nina hakika wanapewa typed report,hii ni kimdhalilisha mtoa report.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...