Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akikata utepe kuashiria ufunguzi ward ya wajawazito katika hospitali ya Rufaa Bugando jijini Mwanza ambapo CRDB iliifunga kwa muda ward hiyo ilikuifanyia ukarabati madhubuti na kuwa ya kisasa zaidi. Kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Ilemela Bi. Amina Masenza, Mkurugenzi wa BMC Prof. Charles Majinge, Mkurugenzi mtendaji wa CRDB Dr. Charles Kimei (aliyenyanyua mkono), Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga na mmoja kati ya maafisa wa CRDB. 
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Evarist Ndikilo akifungua pazia la bango la wadhamini katika hafla ya kukabidhi ward ya wajawazito Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza iliyokarabatiwa na CRDB Benki. 
"Tukio hili tunalifanya ikiwa ni hatua za kurejesha kiasi cha fungu la faida kwa jamii, afya ya  jamii inapoimarika ndipo watu wake wanapopata nafasi ya kufanya kazi na kuwekeza kwenye mabenki yetu na hapo ndipo faida inapopatikana"

"Jamii inapokuwa dhoofu kiafya basi kazi nazo haziendi, uwekezaji wa tija unapungua na faida inakosekana, hivyo tumeamua kuwekeza katika kuboresha afya ya jamii ili tuzidi kupata faida" kauli ya Dr. Kimei.
   
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...