Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiki akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree jana. Ili kuweza kupata hotuba za maneno na picha za video unatakiwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678, pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumia www.simu.tv/nyerere mobile tv. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Push Media Mobile Freddie Manento.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Push Media Mobile, Freddie Manento (kushoto) na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku wakibadilisha mkataba mara baada ya kusainiwa katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree. Huduma hiyo inamwezesha mwananchi kupata hotuba mbali mbali mbali za marehemu Baba wa Taifa kwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678. Pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumia www.simu.tv/nyerere mobile tv.
Wafanyakazi wa kampuni ya Push Media Mobile na Taasisi ya Mwalimu Nyerere wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua huduma ya kumwezesha mwananchi kupata hotuba mbali mbali mbali za marehemu Baba wa Taifa kwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678. Pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumia www.simu.tv/nyerere mobile tv.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. It is probably a waste of time. Kusikiliza ni tofauti na vitendo vyetu vya sasa maana ufisadi ndiyo sera haswa. Tafadhali tumuache apumuzike kwa amani. Tumeisha move on!!

    Tuwe wakweli jamani!!

    ReplyDelete
  2. hebu ziwekeni na za raisi wa zanzibar KARUME kwani wote walikua ni viongozi wa TANZANIA. na hata kwenye hela zetu picha yake imo kwenye shillingi mia tano na shilingi mia mbili.

    ReplyDelete
  3. serikali yetu ya mapinduzi ya zanzibar na sisi tuwekeeni hotuba za Mzee Karume kwani tunazipenda sana. tunaomba ombi jamani sie wafrika wa visiwani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...