Eneo la tukio Washington DC ambapo Omar Sykes (picha ya ndani) aliuawa.
Photo Credits: National Review Online

Jumanne wiki hii, idara ya Polisi Washington DC (Metropolitan Police Department) ilitangaza kukamatwa kwa mtuhumiwa mmoja kati ya wawili waliokuwa wakitafutwa kwa mauaji ya mwanafunzi mTanzania aliyekuwa akisoma katika chuo kikuu cha Howard hapa jijini.
Omar Sykes (22) aliuawa usiku wa Julai 4 mwaka huu nje kidogo ya maeneo ya chuo hicho alipokuwa pamoja na mwenzake.

Wakiwa mtaa mmoja toka chuoni, wanafunzi hao walivamiwa na watu wenye silaha waliotaka kuwapora, na katika harakati hizo, Omar alipigwa risasi kifuani na kufariki.

Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC
Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 19, 2013

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Bora polisi wa D.C. wamefanya kazi yao. Je, walioua wale waTanzania Walter Mazula na Mchumba wake wamekamatwa?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...