Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(kulia) akimvisha Cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunura ambaye anahudumu kazi ya Ulinzi wa Amani katika Jimbo la Darful - Sudan. Hafla ya uvalishaji cheo imefanyika leo Oktoba 30, 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
  Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja( kulia) akimpongeza Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunura mara baada ya kumvisha cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam. Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunura ni miongoni mwa Maafisa wa Jeshi la Magereza ambao wanahudumu kazi ya Ulinzi wa Amani katika Jimbo la Darful - Sudan.

  Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza nchini walioshiriki hafla fupi ya uvishaji cheo kwa Afisa Mwandamizi wa Jeshi la Magereza ambaye amevishwa cheo cha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani).
  Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa nasaha fupi mara baada ya zoezi la uvalishaji cheo kwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunura( hayupo pichani) ambaye kwa sasa anahudumu kazi ya Ulinzi wa Amani katika Jimbo la Darful - Sudan.
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Dkt. Kato Rugainunura(aliyesimama) akitoa neno la shukrani kwa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja(hayupo pichani) mara baada ya zoezi la uvalishaji cheo lililofanyika leo Oktoba 30, 2013 katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam( Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...