Mwenyekiti
wa Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama ya Jijini Dar, Emanuely Shedo
maarufu kama 'MC Fomafoma' akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani) juu ya tamasha la uzinduzi wa CD na DVD yao ambayo inaenda na
kwa jina la 'Namtangaza Kristo' ambayo itafanyika tarehe 13/10/2013
kwenye kanisa lao lililopo Kijitonyama, Dar. Kutoka Kulia kwake ni
Mwimbaji Modesti Mogani, Mwimbaji na Mtunzi Oliver Israel.
Kutoka
Kulia ni Meneja Mipango wa Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama, Onai
Joseph, Mwenyekiti wa Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama, Emanuely Shedo
maarufu kama 'MC Fomafoma', Mwimbaji Modesti Mogani, Mwimbaji na Mtunzi
Oliver Israel.Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama jijini Dar es Salaam
inatarajia kufanya tamasha la uzinduzi wake wa albamu 'Namtangaza
Kristo' kwa CD na DVD.
Akizungumza
katika mkutano na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti
wa Kwaya, Emanuely Shedo alisema nia na madhumuni yao ni kufanya tamsaha
la uzinduzi wa kwaya utakaoendana na Jublee.
Aliongeza
kuwa siku hiyo kutakuwa na live bendi pamoja na kwaya nyingine ambazo
zitaungana nao. DVD na CD zitauzwa siku hiyo pamoja na fulana za
'Namtangaza Kristo' ikiwemo pia Key Holder za Kijitonyama. Msikose watu
wote hakuna kiingilio (Itakuwa ni bure kabisa).
Wanakwaya wa Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama wakitoa burudani mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani).Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Ninapenda sana hii kwaya. Wana upako kwa kweli na wanazidi kumeremeta.
ReplyDeleteTuwekeeni kiduchu kwenye youtube na sisi wabeba box ughaibuni angalau tuone na kuiagiza moja kwa moja toka DSM.
ReplyDeleteHalo Ankali.
ReplyDeleteKuna mdau hapo juu ameomba aone japo kiduchu wimbo wa Kwaya kwenye albamu itayozinduliwa Jumapili tarehe 13 Oktoba 2013 .Anaweza kufatilia kwenye link http://www.youtube.com/watch?v=KDRchIZrX1U