Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa upigaji kura wa Azimio nambari A/68/L4 linaloitaka Marekani kuiondolea Cuba Vikwazo vya Kiuchumi, Kibiashara na Kifedha. Pembeni ni Naibu Muwakilishi wa Kudumu, Balozi Ramadhan Mwinyi. Nchi 188 kati ya nchi 194 ambazo ni Mwanachama wa Umoja wa Mataifa zilipiga kura ya ndiyo kuunga mkono azimio hilo katika mkutano uliofanyika siku ya Jumanne hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa zikiwamo nchi zote za Jumuiya ya Ulaya ilihali Marekani na Israel zilipiga kura ya hapana huku nchi tatu ambazo ni Marshall Island, Micronesia na Palau zilipiga kura ya kutofungamana na upande wowote.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...