Familia ya Yagaza ya Korogwe, Tanga inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Mwl. Osckar Yagaza uliotokea siku ya Jumatatu, Oktoba 28, 2013. Shughuli za mazishi zitafanyika siku ya Alhamisi Novemba 7, 2013 nyumbani kwao Manundu Korogwe.
Wana-Yagaza USA watakuwa na mjumuiko wa sala ya Misa Takatifu kumuombea marehemu siku ya Ijumaa Novemba 1, 2013 saa 11 jioni nyumbani kwao 16 Robinson Street Binghamton, NY.
Raha ya milele umpe ee Bwana na mwanga wa milele umuangazie apumzike kwa amani, amina."
Asante sana kwa msaada wako, pamoja na ujumbe huu ninaambatanisha picha ya marehemu.
Kwa niaba ya familia ya Yagaza,
Elizabeth.
914-396-0403
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...