Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na wafanyakazi wa Swissport katika uwanja wa ndege wa kimataifa ya Julius Nyerere wakati akielekea kwenye ndege jioni ya jana, Jumatatu, Oktoba 28, 2013, kwenda London, Uingereza, kwa ziara ya kikazi ya siku nne ambako atahudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Serikali Uwazi (Open Government) uliotishwa na Serikali ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa David Cameroun. Kushoto kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe na kulia kwake ni Meneja wa Shirika la ndege la Emirates uwanjani hapo Bw. Aboubakar Jumaa. (PICHA NA IKULU)
Home
Unlabelled
RAIS KIKWETE ZIARANI NCHINI UINGEREZA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Inaonekana hapa kama vile mheshimiwa Rais na msafara wake hakutumia ndege yake badala yake emirates halafu yuko kwenye hii terminal ya abiria kawaida. Big up Mr.President kwa kubana matumizi ya serikali.
ReplyDeleteNadhani ndege ya Raisi ipo matengenezo.
ReplyDeleteMara zote sisi Tanzania Raisi wetu ni mmoja wa Maraisi wachache ktk Afrika ambao wanatumia Presidential Jet.
Na pia tusichukulie kitendo cha kutumia Ndege ya Raisi ni anasa, la hii pia ni Heshima ya kuwa nchi yetu si haba angalau tunajiweza!!!
Tukumbuke ndege ya Raisi ina vitu vitatu vinavyotujengea heshima.
1.Nembo ya nchi (Adam na Hawa),
2.Bendera ya nchi mkiani,
3.Jina la nchi.
Ndege ya Raisi itengenezwe haraka sana!!!,,,tafadhali.
leo ninaona msafara wamaraisi unapitaa hapa silver town ila uzuri wa ulayaa utapwea escort hakuna mambo ya kusimamisha magari hapaa...kama tz kutiliana hasara za kijinga..
ReplyDeleteRais anajitahidi anastahili usafiri ktk mizungunko yake kwa maslahi ya nchi.lakini namshauri akemee RUSHWA .vinginevyo maendeleo ya nchi ni kama kuweka maji kwenye ndoo inayo vuja.
ReplyDelete