Washiriki wa mkutano wa 7 wa Mapitio ya Utendaji wa sekta ya Uchukuzi, wakijitambulisha kabla ya mkutano huo wa siku mbili kuanza katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Jubilee. Mkutano huo  wa 7 unawakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta na kuzitafutia ufumbuzi.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa Mkutano 7 wa mapitio ya utendaji wa Sekta ya Uchukuzi(JTSR 2013), unaofanyika katika ukumbi wa mikutano Jengo la Golden Jubilee tarehe 28-29 Oktoba 2013. Mkutano huo wa 7 unawakutanisha wadau mbambali wa sekta ya uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya uchukuzi na kuzitafutia ufumbuzi ili kuboresha Uchukuzi nchini Tanzania.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Alhaj Mussa Iyombe, akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa Sekta ya Uchukuzi leo asubuhi katika ukumbi wa mikutano katika Jengo la Golden Jubilee.
 Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi leo asubuhi katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye Jengo la Golden Jubilee(PSPF BUILIDNG). Mkutano huo wa siku mbili unakutanisha wadau wa taasisi mbalimbali za sekta ya uchukuzi kujadili njia mbalimbali za kuboresha sekta ya Uchukuzi.

 Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe (wa tatu kutoka kushoto waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi, wahisani wa Miradi ya Maendeleo na wajumbe mbalimbali waliohudhuria mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi, Unaofanyika tarehe 28-29 Oktoba katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Golden Jubilee. Wa kwanza kushoto waliokaa ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mrs. Monica Mwamunyange, kulia kwa Waziri Mwakyembe ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka.
Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Usimamizi, Ufuatiliaji na Tathimini wa Wizara ya Uchukuzi , Bw. Aunyisa Meena, akiwasilisha mada kwenye mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi, unaofanyika Tarehe 28-29 Oktoba katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Golden Jubilee. Mkutano huo utajadili maswala mbalimbali yanayohusu sekta ya Uchukuzi.
Habari na picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...