Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki Prof. Keto Mshigeni, anapenda kuwaalika wahitimu wote wa mwaka wa masomo wa 2012/2013, wazazi, walezi wadau mbalimbali, wananchi na waandishi wa habari,  kwenye sherehe za Mahafali ya Kumi  na Moja, zitakazofanyika Jumamosi, tarehe 2 Novemba 2013, katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, kuanzia Saa 3:30 Asubuhi.

Mgeni rasmi atakuwa ni Mkuu wa Chuo, Mheshimiwa Dk. Salim Ahmed Salim, ambaye pia atatunuku vyeti, shahada, na stashahada kwa wahitimu.

Wananchi wote mnakaribishwa kwenye mahafali hayo.
Tangazo hili limetolewa na:
                  Ofisi ya Makamu Mkuu wa Chuo,
      Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki,
S.L.P.  65300, Dar es Salaam, Tanzania
Simu: +255 22 2700021/4, Mob:0764378755

        Faksi: +255 22 2775591,  Barua pepe: secvc@hkmu.ac.tz   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...