Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Albinus Mugonya akiwakaribisha Madiwani 12 wa Manispaa  ya Musoma (kulia) waliongozana na baadhi ya watumishi sita kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya. Msafara huo umefika Mkoani Rukwa kwa ziara ya kujifunza mambo mbalimbali ya kiuongozi kutoka kwa madiwani wenzao wa Manispaa ya Sumbawanga na Serikali ya Mkoa kwa ujumla.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Sabas Katepa akiwatambulisha madiwani mbalimbali kutoka Manispaa ya Musoma Mkoani Mara walipofika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa ajili ya utambulisho katika ziara yao ya mafunzo Mkoani Rukwa. 
Madiwani hao walipata fursa ya kutembelea ukumbi wa kurushia mawasiliano ya moja kwa moja (Video Conference) ambayo yanauwezo wa kuziunganisha ofisi mbalimbali za Serikali katika kikao kimoja. Pichani Mchambuzi wa mifumo ya Kompyuta Galus Ouma akitoa maelezo mafupi na namna mtandao huo unavyofanya kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...