Mzee Mandela na mkewe Winnie Mandela wakiwasili Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mwaka 1990, siku chache baada ya Madiba kuachiliwa huru kutoka gerezani na kabla hajawa Rais wa Afrika ya Kusini. Tanzania ilikuwa nchi ya kwanza kuitembelea baada ya kuachiwa huru ikiwa ni kutoa shukrani kwa msaada wa hali na mali aliopokea toka Tanzania wakati wa kugombea ukombozi wa Afrika Kusini
 Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere akiwatambulisha Nelson Mandela na Winnie Mandela kwa Watanzania Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mwaka huo wa 1990
 Waziri Kiongozi wa Zanzibar wa wakati huo, Marehemu Dr. Omar Ali Juma, akiwalaki Madiba na Winnie Mandela walipotembelea visiwani mwaka huo wa 1990
 Maelfu ya wananchi wa jiji la Dar es salaam walijitokeza kumlaki Nelson Mandela na Winnie Mandela alipotembelea Tanzania mara baada ya kutoka kifungoni mwaka 1990. Ankal, ambaye ndiye aliyenasa taswira zote hizi, anaikumbuka hii siku kama ya kihistoria kwake kwani ndio ilikuwa kazi yake kubwa ya kwanza toka ajiunge na gazeti la Daily News. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Tanzania hatukuanza harakati za Ukombozi leo hii kwa kutuma Vikosi Vitani Congo-DRC kuwasakaka Waasi!

    Rwanda na Uganda mliokereka na Operesheni ya Majeshi yetu JWTZ-UN BRIGADE huko DRC habari ndiyo hiyo, mtu wa UZAO wetu Jemadari Mpiganaji mwenzetu Mzee Madiba ndio huyooo ameaga dunia...Tanzania tunasikitika tunaomboleza!

    Kama inavyoonekana Kidume Mzee Madiba anachomoka Lupango moja kwa moja anawaona Wapiganaji wenzake TANZANIA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...