Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Mkazi, Mhe. Goodluck Ole Medeye, akikabithi tuzo ya mshindi wa kwanza ya hesabu bora za mwaka 2012 katika sekta ya hifadhi ya jamii iliyochukuliwa na Mfuko wa Pensheni wa LEPF ambapo ilipokelewa na Mkurugenzi wa Fedha wa Lapf, John Kida. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa NBAA, Pius Maneno. Sherehe hizo zimefanyika jana usiku katika hoteli ya Naura Springs mjini Arusha.
Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, John Kida, mwenye tuzo, akionyesha Tuzo ya Ubora wa mahesabu kwa wafanyakazi wa LAPF mara baada ya kukabidhiwa. Kutoka Kushoto ni Mhasibu Mkuu wa LEPF, Rock Massawe, Meneja Kanda ya Kaskazini, Rajab Kinande, na kulia ni mtumishi wa LEPF Arusha, Flowin Ngonyani wakati wa sherehe za kukabidhiwa tuzo za NBAA zilizofanyika jana usiku katika hoteli ya Naura springs, Arusha.
Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF, John Kida, mwenye tuzo, akizungumza na waandishi wa habari, (hawapo pichani) mara baada ya kukabidhiwa tuzo ya NBAA ya ubora wa mahesabu kwa sekta za hifadhi za jamii. Kulia ni Afisa Masoko wa LAPF, Rehema Mkamba na Kushoto ni Mhasibu Mkuu wa LAPF, Rock Masawe wakati wa sherehe za kukabidhiwa tuzo za NBAA zilizofanyika jana usiku katika hoteli ya Naura springs, Arusha.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...