WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amelipongeza Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Arusha kwa kubuni na kuunda Umoja wa Madhehebu ya Kikristu katika mkoa wa Arusha kama njia ya kuleta amani na mshikamano kwa waumini wake.
Ametoa pongezi hizo leo mchana (Jumapili, Desemba 29, 2013) wakati akitoa salamu za Serikali kwenye ibada ya kuadhimisha Jubilei ya miaka 50 ya Jimbo Kuu Katoliki la Arusha iliyofanyika kwenye viwanja vya Kanisa Kuu la Mt. Theresia wa Mtoto Yesu jijini Arusha.
Waziri Mkuu ambaye alishiriki ibada hiyo kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete, alisema uamuzi uliofanywa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Arusha, Mhashamu Josaphat Lebulu ni wa kuigwa na viongozi wa mikoa mingine kwani unasaidia kuwaunganisha viongozi wote bila kujali tofauti zao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...