Washitakiwa wanne kati ya watano kutoka kushoto juu hadi wa nne wakiwa wanatoka mahakamani chini ya ulinzi mkali.
Ulinzi ukiimarishwa Baada ya watuhumiwa wa ujambazi kufikishwa mahakamani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Anayetenda kosa kulingana na sheria tulizonazo ni haki kupelekwa mahakamani na kuhukumiwa bila kujali cheo n.k.

    ReplyDelete
  2. Hii Kasi ya Maisha bila kutumia akili, busara na utulivu itatufanya wengi wenye pupa ya kufikia malengo ya kimaisha kuishia Magerezani!!!

    Jamaa hao wanne wanaonekana Masharo kiaina na Mabraza, yaani mmeshindwa kutambua ya kuwa Shetani anawahujumu hadi mkiuke?

    ReplyDelete
  3. Aibu gani hii?

    Yaani Maafande pamoja na kula Kiapo cha utii wakati mnahitimu Mafunzo ili kuitumikia nchi na leo mmetumia akili finyu mmeshiriki Ujambazi na sasa mpo chini ya Mkono wa Mamlaka ya Sheria!

    Mlitakiwa ninyi kuwa ndio wa kuwaelimisha umma wa wananchi kuacha Uhalifu na Ujambazi!!!

    Mmeonyesha upeo mdogo wa kiakili wa kutafuta mafanikio kwa njia za mkato na haraka haraka ilhali Fursa nchini zipo lukuki.

    Sasa leo hii nyie ndio wajinga wenyewe, ohhh kama ardhi ingekuwa na mfuniko nadhani Maafande wangeomba ardhi ifunguke wajisitiri kwa aibu!

    ReplyDelete
  4. Inaonyesha Maafande walisha fanikisha mara kadhaa huko nyuma kabla na leo hii 40 yao imetimia na wamenaswa!

    ReplyDelete
  5. Maafande Wahalifu mmejikuta mpo chini ya Ulinzi mkali wa Maafande wenzenu!

    Ni jambo la aibu na huruma lakini bahati mbaya Sheria haina Huruma, aibu na bahati mbaya!

    Wala Sheria haina nilikuwa sijui, nimeghafirika, wamenidanganya !!!

    ReplyDelete
  6. Hiyo ndio slogani ya changamkia fursa. Walizimana hawa, wenzao waka wakomoa, huwa wanakuwa timu kubwa, wakuiba na wakuzuia wenzao wasiwahi sehemu ya tukio.

    ReplyDelete
  7. HAO SIO WA KUWAONEA HURUMA HATA KIDOGO.HAO NI SAWA NA MBWA

    Ankal samahani sana nimetumia lugha kali hapo juu sababu hawa jamaa wanatia hasira sana.Naomba usinitupie kapuni oni langu.Nilikuwa nafikisha ujumbe kwa wengineo ambao wapo uraiani na wanaendelea au wanafanya ujambazi.

    ReplyDelete
  8. Enhhh huyo Jambazi mwenye Mgolole wa shuka la drafti ni mwana Chadema?

    Chadema fanyeni jitihada kumunya'nganya huo mgolole mabegani huyo Mtuhumiwa wa Ujambazi ni vile anakichafua chama chenu!

    ReplyDelete
  9. Hawa ni watu wabaya sana !

    Yani unabeba Biblia ama Msahafu wakati wa Kiapo cha Utii ili kulitumikia Jeshi, wananchi na Taifa, halafu leo ndio wewe wewe tena unabeba silaha unaugeuza mtutu wa bunduki kwa wananchi?

    ReplyDelete
  10. Huu sio utaratibu mzuri wa police kuwa na silaha bila ya kuvaa uniform, raia wa kawaida wanaweza kutumia mfumo huu kama majambazi kwa kuji pretend as police kwa kuvaa ngu za kawaida. Inaonekana sasa kuwa mazeoa kwa jeshi la police.

    Police lazima wawe professional wanapokuwa kazini, sio wamevaza nguo kama wanaenda club.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...