Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Rais Mstaafu wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi,alipohudhuria katika Uzinduzi wa Taasisi ya Mwanaharakati Bibi Siti Binti Saad,katika ukumbi wa Salama Hall Bwawani Hotel jana,ikiwa ni miongoni mwa shamra shamra za miaka 50 ya mapinduzi Ya zanzibar (katikati) Bibi Nasra Mohamed Halal Mwenyekiti wa Taasisi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na kumpongeza Dk.Amina Ameir,baada ya kutoa Historia ya Harakati za wanawake katika uzinduzi wa Taasisi ya Mwanaharakati Bibi Siti Binti Saad katika ukumbi wa Salama Hall Bwawani Hotel Mjini Unguja jana,ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mzee Ali Hassan Mwinyi,(akiyesimama) akiwa mlezi wa Taasisi ya Mwanaharakati Bibi Siti Binti Saad,akimkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,kuizindua taasisi hiyo katika ukumbi wa Salama Hall Bwawani Hotel Mjini Unguja jana,ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akizungumza na Viongozi na wananchi wakati alipozindua Taasisi ya Mwanaharakati Bibi Siti Binti Saad katika ukumbi wa Salama Hall Bwawani Hotel Mjini Unguja jana,ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.
KWA ZAIDI YA MIAKA SITINI SITI BINTI SAAD AMEKUWA AKIJULIKANA KUWA NI MWANAMUZIKI KWA MOJA YA WIMBO WAKE 'MAZOEA YANA TABU' NI KWANINI HAKUWAHI KUTAMBULISHWA UANAHARAKATI NA WASHIRIKA WAKE NI NANI PIA KIPINDI CHA HARAKATI ZAKE NI KIPI. NI VIZURI WANANCHI TUJULISHWA KUMBUKUMBU HIZI BADALA YA KUAMBIWA TU KUWA NI MWANAHARAKATI.
ReplyDelete