NA ABDULAZIZ VIDEO,Kilwa
Halmashauri ya wilaya ya Kilwa imeomba kuidhinishiwa jumla ya Tshs
28,729,895,535 kwa ajili ya Uendeshaji wa shughuli mbalimbali za
serikali ikiwemo Mishahara Tshs 14,016,723,484 huku mapato ya ndani
ni Tshs 268,112,400 na matumizi mengineyo (OC)ni 1,567,578,000 toka
serikali kuu na mapato ya ndani 2,054,184,359
Aidha Miradi ya maendeleo tshs 2,994,804,988 toka serikali kuu na
wahisani 409,817.075 na mapato ya ndani Tshs 10,823,297,292
Akisoma bajeti hiyo katika kikao cha Baraza maalum la bajeti kwa
Madiwani wa Halmashauri hiyo,Afisa Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya
Kilwa,Daniel Lusingu alibainisha kuwa Bajeti hiyo ina ongezeko la
jumla ya Tshs 8.866,528,435 sawa na asilimia 44.63 ya bajeti ya mwaka
2013/2014
Pamoja na maombi hayo ya kuidhinishiwa mapato na matumizi Halmashauri
ya wilaya ya Kilwa katika kuhakikisha inaongeza mapato kutoka katika
vyanzo vya ndani imejipanga kuongeza wigo baada ya kubuni vyanzo vipya
ikiwemo kuongeza wigo wa ukusanyaji kodi mbalimbali, Kuimarisha
Uagizaji na utunzaji wa nyaraka za kukusanyia mapato na kuimarisha
rejesta ya vyanzo vya mapato
Sambamba na kuongeza wigo wa ubinafsishaji wa vyanzo na kufanya
uhakiki kila mara pamoja na kutoa elimu kwa walipa kodi na kuongeza
nguvu kwenye kudhibiti mazao yatokanayo na bahari,kilimo na misitu kwa
kusimamia kwa karibu vizuizi katika maeneo ya
Singino,Migeregere,Mbwemkuru,mihangalaya na Nanjirinji
Akichangia bajeti hiyo,Diwani wa kata ya Songosongo,Mhe Hassan Swaleh
pamoja na kuunga mkono Bajeti hiyo aliiomba Halmashauri hiyo kuona
umuhimu wa kuthamini wavuvi kwa kupatiwa zana bora za uvuvi Ili
kuongeza wigo katika makusanyo ya baharini
Madiwani wakiwa katika kikao cha kupitisha bajeti kinachoendelea katika ukumbi wa Jumba la maendeleo wilayani Kilwa
Madiwani wakiwa katika kikao cha kupitisha bajeti kinachoendelea katika ukumbi wa Jumba la maendeleo wilayani Kilwa
Afisa Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya kilwa ,Daniel Lusingu akiwasilisha makisio ya bajeti ya Halmashauri hiyo
Wakuu wa Idara wa Halmashauri wakihudhuria kikao hicho
Meza Kuu. Picha zote na Abdulaziz Video
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...