JESHI LA POLISI
MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU 08
WOTE RAIA NA WAKAZI WA SANGE – BUKAVU NCHINI KONGO WAKIONGOZWA NA HESABU LUHIGITA (16) BAADA YA KUINGIA
NCHINI BILA KIBALI.
WATUHUMIWA HAO WALIKAMATWA MNAMO TAREHE 12.02.2014 MAJIRA YA SAA 13:00HRS MCHANA HUKO KATIKA KIJIJI
CHA IKUMBILO WILAYA YA ILEJE WAKIWA WANASAFIRISHWA KWENYE GARI LENYE NAMBA ZA
USAJILI T.136 AQC AINA YA FUSO
LILILOKUWA LIKIENDESHWA NA MUSSA DISI
(35) NA MATEO KADUMA (30) WOTE WAKAZI WA ISONGOLE AMBAO PIA WAMEKAMATWA PAMOJA
NA GARI HILO.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA
POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO
KWA JAMII KUENDELEA KUTOA TAARIFA KWA JESHI LA POLISI KUHUSIANA NA MTU/WATU
WANAOWATILIA SHAKA IKIWA NI PAMOJA NA RAIA WA KIGENI ILI HATUA ZA KISHERIA DHIDI YAO ZICHUKULIWE.
Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...