Na Andrew Chale

KAMPUNI ya uuzaji wa bidhaa za majumbani na ofisini ya Home Shopping Centre (HSC) imemzawadia mshindi wake wa kwanza wa ‘pendezesha nyumba na HSC’, Rehane Jaffer zawadi ya sh 500,000.  Shindano hilo linaendeshwa kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook kwa  jina la ‘Give a Way’. 
Mshindi alikabidhiwa hundi ya kiasi hicho cha pesa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Meneja Mauzo na Masoko wa HSC, Nadhir Mubarak Bahayan ambaye aliwataka watanzania kushiriki shindano hilo ambalo kila Ijumaa watakuwa wakijishindia sh. 500,000. 
 “Wateja wetu wa HSC, wanatakiwa kujiunga kwenye mtandao wetu wa facebook na kisha kututumia picha walizopamba ndani ya nyumba zao zitokanazo na bidhaa zetu,” alisema Nadhir. Alisema shindano hilo litaendeshwa kwa mwezi mzima wa Machi 2014
 . 
Mshindi huyo aliipongeza HSC kwa shindano hio na kusema ni faraja kwake na familia yake. Aidha zoezi hilo ambalo litaendeshwa kwa muda wa mwezi mzima wa Machi huku kila Ijumaa ikitarajiwa kutangaza washindi na kukabidhiwa hundi siku inayofuata. 
 Nadhir aliwataka wateja wao kuwa na tabia ya kutembea kwenye mtandao wa HSC, na kushiriki kupitia https://www.facebook.com/hsctz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...