MKURUGENZI wa Mashitaka Nchini (DPP), amemfutia mashitaka aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Gabriel Fuime (61) na kisha kumuunganisha na wenzake 11 na kuwasomea upya mashtaka 27 ya mauji katika mtaa wa Indira Gandh, yaliyotokana na kuporomoka jengo la ghorofa 16.
Mbali na Fuime washtakiwa wengine ni, Diwani wa Kata ya Goba, Ibrahim Mohamed maarufu kama Kisoki, Raza Ladha, Goodluck Mbanga, Willbroad Mugyabuso,Mohamed Abdulkarim, Charles Ogare, Zonazea Oushoudada, Vedasto Ruhale, Michael Hema, Albert Mnuo na Joseph Ringo.
Washtakiwa hao walisomewa hati mpya ya mashitaka baada ya kuondolewa hati ya zamani ya mauaji ya bila kukusudiwa na kuunganishwa Fuime na idadi yao kufikia 12, mbele ya Hakimu Mkazi Devota Kisoka.
Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Benard Kongola akisaidiana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka na Wakili wa Serikali Joseph Maugo.
Kongola alidai kuwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha 294 kidogo cha (1) upande wa Jamhuri unaomba ridhaa ya mahakama ya kumuongeza mshtakiwa Fuime katika hati mpya ya mshitaka.
Hakimu Kisoka alisema mahakama haina pingamizi na maombi ya Jamhuri ya kubadilisha hati ya mashitaka dhidi ya washtakiwa.
Jamhuri ilidai kuwa katika shtaka la kwanza, Machi 29, mwaka 2013 mtaa wa Indira Gandh, Wilaya ya Ilala washtakiwa kwa pamoja walimuua kwa makusudi Yusuph Khari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...