Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi alipowasili katika viwanja vya CCM Kisiwandui leo katika hitma na dua ya Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume.
Mke wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume akitia ubani wakati wa hitma ya kumuombea dua Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,iliyosomwa leo katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja,wengine pia ni wake wa Viongozi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein wakisalimiana wajukuu wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume,na Viongozi wakati wa hitma na dua iliyoombwa na wananchi wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar leo mchana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) akiungana na Viongozi,Wananchi katika kumuombe dua kwa Kisomo cha Hitma iliyosomwa leo katika Ukumbi wa CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar,wakiwemo Rais wa Tanzania Alhaj Dk.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais mstaafu wa Tanzania Mzee Mwinyi,Rais mstaafu wa Zanzibar Dk.Amani Abeid Karume,Makamo wa Rais wa Tanzania Dk.Bilali,Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Viongozi wengine (wa pili kushoto).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...