Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) akipokea ufunguo ikiwa ishara ya kukabidhiwa magari matano kutoka kwa Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada wakati wa tafrija fupi ya makabidhiano ya magari hayo kutoka Serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika majukumu yake ya kuzima moto na uokoaji nchini. Makabidhiano hayo yalifanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (kulia) na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada wakikata utepe ikiwa ishara ya makabidhiano ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini. Magari hayo yamekabidhiwa katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam.  Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akiikagua  moja ya magari matano yaliyotolewa na Serikali ya Japan kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Magari hayo matano yalitolewa na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada wakati wa tafrija fupi ya makabidhiano ya magari hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akitoa hotuba fupi ya kuishukuru Serikali ya Japan kwa kuisadia wizara yake kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji magari matano kwa ajili ya kazi ya kuzima moto na uokoaji nchini. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada ambaye alikabidhi magari hayo kwa niaba ya Serikali yake. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha. makabidhiano ya magari hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam leo. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamishna Jenerali Pius Makuru Nyambacha akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (katikati) ili aweze kuzungumza na baadaye kukabidhiwa magari matano ya kuzima motona uokoaji. Magari hayo yametolewa na Serikali ya Japan kupitia balozi wake nchini, Masaki Okada (kushoto) katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya
 
Taswira ya magari matano yaliyokabidhiwa na Balozi wa Japan, Masaki Okada kwa niaba ya Serikali yake. Magari hayo matano yaliyotolewa kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji yalipokelewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto Kanda ya Ilala, jijini Dar es Salaam. Picha zote na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI WIZARA YA MAMBO YA NDANI 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...