Bw. Stanley Bergman akiteta jambo na Balozi Manongi wanaonekana pia wageni waalikwa waliojitokeza kwa wingi kwenye hafla hiyo.
Rais na Mwanzilishi wa MCW, Bw. Eddie Bergman akielezea historia ya Taasisi hiyo ambayo aliianzisha ( 1999) akatumia fursa hiyo kutoa shukrani zake kwa wadau , wafadhili na marafiki mbalimbali ambao wameendelea kuiwezesha Taasisi hiyo na hatimaye kupitia kwayo kusaidia jamii katika maeneo mbalimbali na uwezeshaji wa vijana.
Bw. Stanley Bergman, Mwenyekiti na CEO, Henry Schein Inc akizungumza wakati wa hafla ya miaka kumi ya uchangiaji wa Taasisi ya Miracle Corners of the World ( MCW) ambayo pia imetimiza miaka kumi na tano ya kuanzishwa kwake, katika mazungumzo yake alitoa shukrani na pongezi kwa Mhe. Rais Jakaya Kikwete kwa namna ambayo amekuwa akishirikiana na Taasisi hiyo ambayo inaendesha shughuli hususani uboreshaji na uimarishaji wa huduma ya afya ya kinywa.
Mhe. Balozi Tuvako Manongi Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akisema machache wakati wa hafla hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...