Mkuu wa Bandari ya Mtwara, Absalom Bohela (kushoto) akikabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Ludovick Mwananzila (kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika hivi karibuni katika kijiji cha Mahumbika kilichopo Lindi vijijini. 
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Ludovick Mwananzila (kulia) na Mkuu wa Bandari ya Mtwara, Absalom Bohela (kushoto) wakiwa na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mahumbika wakati wa kukabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwa shule za mkoa wa Lindi hivi karibuni.
 Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Mahumbika wakifurahia jambo wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), iliyofanyika hivi karibuni katika kijiji cha Mahumbika kilichopo Lindi vijijini.
 Wasanii wa kikundi cha ngoma na maigizo cha kijiji cha Mahumbika, Lindi wakitoa burudani wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), iliyofanyika hivi karibuni katika kijiji cha Mahumbika kilichopo Lindi vijijini.
 Msanii wa kikundi cha ngoma na maigizo cha kijiji cha Mahumbika, Lindi akitoa burudani wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), iliyofanyika hivi karibuni katika kijiji cha Mahumbika kilichopo Lindi vijijini.
 Mkuu wa Bandari ya Mtwara, Absalom Bohela akisoma hotuba kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kabla ya kukabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Ludovick Mwananzila hivi karibuni. 

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), imekabidhi msaada wa madawati 110 yenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa shule za Mkoa wa Lindi katika hafla iliyofanyika hivi karibuni katika kijiji cha Mahumbika kilichopo Lindi vijijini. Msaada huo wa madawati umekabidhiwa kwa shule hizo hivi karibuni na mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Bw. Absolom Bohella mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mh. Ludovick Mwananzila.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hongereni TPA. Kwa msaada wa kuleta maendeleo. Mbona makampuni makubwa ya mafuta hayachangii? Au si wenzetu!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...