Meneja Uwekezaji katika Jamii na Udhamini wa Benki ya NBC, Rukia Mtingwa akifanyiwa uchunguzi wa afya ya kinywa na Dk. Asnath Katoto wa Metropolitan Health Insurance, wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya ya benki hiyo ambayo wafanyakazi wa benki hiyo walipimwa vipimo mbalimbali ili kujua hali za afya zao na kupata ushauri. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, Leah Yusuf Mndolwa (kushoto) akitolewa damu ili kupimwa afya yake na Mtaalam wa Maabara kutoka Metropolitan Health Insurance, Scanderia Mambaya wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya ya benki hiyo ambayo wafanyakazi wa benki hiyo walipimwa vipimo mbalimbali ili kujua hali za afya zao na kupata ushauri. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, Cecilia Machaku (kushoto) akifanyiwa uchunguzi wa afya yake katika zoezi hilo jijini Dar es Salaam. Anayempima ni Dk. Asnath Katoto wa Metropolitan Health Insurance.
Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya NBC, Leah Ntambula (kushoto) akipimwa msukumo wa damu (BP) na Dk. Asnath Katoto wa Metropolitan Health Insurance wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya ya benki hiyo ambayo wafanyakazi wa benki hiyo walipimwa vipimo mbalimbali ili kujua hali za afya zao na kupata ushauri.
Meneja wa Benki ya NBC, Tawi la Corporate, Godfrey Ndossa (kushoto) akipimwa uzito na urefu ikiwa ni moja ya vipimo vya afya na Josephine Sempanga's wa Metropolitan Health Insurance wakati wa maadhimisho ya wiki ya Afya ya benki hiyo jijini Dar es Salaam. Kuna uhusiano kati ya uzito na urefu kwa mtu mwenye afya bora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...